Pages

Monday, December 23, 2013

LICHA YA USHINDI WA SIMBA, YANGA WAIBUKA NA KITITA CHA FEDHA


Wachezaji wa Timu ya Simba na baadhi ya viongozi wao wakipozi na kombe lao baada ya kukabidhiwa kwa kuifunga Timu ya Yanga Mabao 3-1 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jioni ya leo.Mabao ya Simba yalifungwa na Hamis Tambwe mawili na Ramadhan Singano huku la kufutia machozi la Yanga likifungwa na Emmanuel Okwi.Picha zote na Othman Michuzi.
Meneja wa Yanga, Afidh Ally akipokea mfano wa hundi ya zaidi sh. 98 milioni Kwa kuibuka washindi katika shindano la Nani Mtani Jembe kwa kupata kura nyingi katika unywaji wa bia ya Kilimanjaro.
Hundi ya Simba ilisomeka hivi pamoja na Ushindi Mkubwa walioupata dhidi ya wapinzani wao.
Mgeni Rasmi katika Mchezo huo,Waziri wa Sheria na Katiba,Mh. Mathias Chikawe akikabidhi Kombe la Ushindi wa Nani Mtani Jembe kwa Nahodha wa Timu ya Simba mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo jioni hii kwenye Uwanja wa Taifa,Jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji wa Timu ya Yanga,Mrisho Ngassa (17),akiwa mpiga chenga ya Mwili Beki wa Timu ya Simba,Donald Mtosi wakati mchezo wao wa Nani Mtani Jembe unaoendelea hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Hadi hivi sasa Simba wanaongoza kwa Bao 1-0 na tayari dakika 35 za mchezo zishakatika.Picha zote na Othman Michuzi.
Golikipa Machachari wa Timu ya Simba,Ivo Mapunda akiruka juu kudaka mpira uliokuwa unaelekea langini kwake.
Simba wakiandika Bao la Kwanza mnamo dakika ya 19 ya mchezo.
 Mashabiki wa Simba.
Nahodha wa Timu ya Simba,Henry Joseph Shindika akikabiliana na Mpinzani wake wakati wa Mtanange wa Nani Mtani Jembe uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,jioni ya leo.
Kelvin Yondani wa Yanga akitoa pasi nzuri.































Friday, December 20, 2013

OKWI ATUA JANGWANI

SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 50 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Daktari dhamana Wilaya ya kusini (DMO) Daniel Francis Pius,(katikati) baada ya kukifungua
kituo cha Afya Kijiji cha Kajengwa Makunduchi, Wilaya ya Kusini Unguja jana,katika shamra shamra  kuadhimisha Miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
 Wasoma Utenzi Amina Makame Omar,na Marium Amour Haji,kutoka Shehia ya Kijini,walipokuwa wakitoa burudani hiyo kwa wananchi wakati wa  ufunguaji  Kituo cha Afya Kijiji cha Kajengwa,Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja jana,katika shamra shamra  kuadhimisha Miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
 Katibu wa Kamati ya maendeleo Shehia ya Kajengwa Makunduchi Nassor Simba,alipokuwa akisoma risala ya wananchi wa kijiji hicho wakati wa  ufunguzi wa  kituo cha Afya Kijiji cha Kajengwa,Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja jana,katika shamra shamra  kuadhimisha Miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
 Baadhi ya Wananchi wa Shehia ya  Kijiji cha Kajengwa Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja,na Vijiji jirani wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akizungumza nao wakati wa ufunguzi  wa Kituo cha Afya Kijiji hapo,katika shamra shamra   kuadhimisha Miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dk.Saleh Mohamed Jidawi,alipokuwa akitoa Taarifa na shukurani wa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,baada ya kukifungua kituo cha Afya cha Shehia ya Kajengwa  Makunduchi,Wilaya ya Kusini Unguja jana,katika shamra shamra   kuadhimisha Miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
 Wafanyakazi wa Kituo cha Afya Kajengwa Makunduchi,Wilaya ya Kusini Unguja,wakiwa sherehe za Ufunguzi wa Kituo hicho,katika kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,sherehe hizo zilifanyika jana,na kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa mgeni rasmi
 Juu na chini: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kajengwa Makunduchi,Wilaya ya Kusini Unguja,jana wakati wa sherehe za ufunguzi wa Kituo cha Afya,katika maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]