Pages

Friday, January 11, 2013

Waasi wa M23 watishia kususia mazungumzo


Mazungumzo ya kuleta amani kati ya kundi la M23 na serikali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yanarejelewa tena hii leo mjini Kampala Uganda.
Mazungumzo hayo yalisitishwa mwaka jana kwa ajili ya sherehe za Krismasi na mwaka mpya.
Hata hivyo vigogo husika kwenye mzozo huo,Rais Joseph Kabila na Jean Marie Runiga kiongozi wa kundi hilo la waasi wa M23 hawatahudhuria mazungumzo hayo.
Kundi hilo la M23 limetishia kujiondoa kwenye mazungumzo hayo hadi pale rais Joseph Kabila atakaposaini mkataba wa kusitisha mapigano.
Msemaji wa serikali ya Congo ameliambia shirika la Habari la Reuters kuwa limepuuza masharti hayo ya waasi kwa kuwa hayana msingi wowote.
Mazungumzo ya kujaribu kutatua mzozo huo uliodumu kwa zaidi ya miezi tisa yaliyofanyika mwaka uliopita yalisambaratika, baada ya wawakilishi wa pande hizo mbili kushindwa kuafikiana.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu laki nane wamekimbia makwao tangu waasi hao kaunzisha vita dhidi ya serikali ya nchi hiyo mwezi Mei Mwaka uliopita, kwa tuhuma za kupuuza mkataba uliokuwa sainiwa awali wa kuwashirikisha katika jeshi la serikali.

Jean-Marie

No comments:

Post a Comment