Imefahamika kuwa lililokuwa kundi maarufu la muziki nchini Uingereza la ‘Spice Girls’ limeungana tena na linatarajiwa kufanya onesho kabambe wakati wa sherehe za kufunga michezo Olimpiki 2012 jiji London.
Hata kabla ya wanamuziki wenyewe wa kundi hilo kuthibitisha habari hizo, tayari kamera za mitandao ya habari zimewanasa wakifanya mazoezi kwa ajili ya ‘show’ ya siku ya Jumapili.
Kikosi kizima cha kundi hilo kinachoundwa na Victoria Beckham, Geri Halliwell, Emma Bunton, Mel C na Mel B wameonekana wakinya mazoezi ya nguvu yanayolenga kuuthibitishia umma uwezo wao.